SAM QUERREY AMSHINDA NOVAK DJOKOVIC


Novak Djokovic amebanduliwa katika mashindano ya Wimbledon baada kushindwa na raia wa Marekani Sam Querrey na hivyobasi kusitisha matumaini ya mchezaji huyo aliye nambari moja duniani kushinda taji la mwaka la Grand Slam.
Querrey,aliyeorodheshwa nambari 28,alishinda kwa seti 7-6 {8-6} 6-1 3-6 7-6 {7-5} katika raundi ya tatu baada ya mvua kusitisha mchezo kwa mda.
Ni mara ya kwanza kwa raia huyo wa Serbia kushindwa katika shindano kubwa tangu 2015 wakati wa fainali za French Open.

Djokovic alikuwa na matumaini ya kushinda taji lake la tatu mfululizo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 tayari ameshinda mataji ya Australia na Ufaransa mwaka 2015.

No comments