TETESI ZA USAJILI ULAYA LEO JUMATATU

Arsenal wanafikiria kutoa pauni milioni 45 kumtaka beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26. (Express)


    Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa amepigwa picha kwenye Instagram akiwa amevaa jezi ya Atletico Marid na kuandika "mpe salaam zangu Conte". (Mail)
    Chelsea wanataka kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Emerick-Aubameyang, 28, baada ya kumkosa Romelu Lukaku, 24. (Sky)

    Chelsea wameonywa na Borussia Dortmund kuwa wana wiki moja tu ya kumsajili Pierre Emerick-Aubameyang. (The Sun)
    Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anadhani kuwa ataweza kumshawishi Alexis Sanchez, kutoondoka Emirates. (Mirror)
    Vinginevyo Arsene Wenger anafikikia kupanda dau kumtaka mshambuliaji wa Celtic, Moussa Dembele, 20. (Star)
    Arsene Wenger amekata tama ya kumsajili Kylian Mbappe, 18, na badala yake sasa anaelekeza nguvu katika kumsajili Thomas Lemar, 21, kutoka Monaco. (Telegraph)
    Arsenal pia wanafikiria kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, kuziba nafasi ya Alexis Sanchez ikiwa ataondoka. (Don Balon)

    No comments