SAMATA AWAPA NENO WACHEZAJI WA BONGO

Nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Mbwana Samata amewataka wachezaji wa Tanzania kuendelea kuwa na nidhamu ya mchezo kwa kuwa nchi hii imebalikiwa kuwa na wachezaji wenye nidhamu ya hali ya juu.


Samata amewataka wachezaji hao kujituma zaidi pale wanapopata nafasi ya kucheza soka la kulipwa nje ya nchi kwani kujituma kwao kutakuwa tija kwa timu ya Taifa kuwa na wachezaji bora.


Alisema kwamba endapo jambo hilo litafanywa kwa kila mchezaji atakaepata nafasi ya kwenda kucheza soka la kulipwa anaamini kila mmoja atafanikiwa zaidi katika soka.

No comments