PAMBANO LA YANGA NA MC ALGER KUCHEZWA MWANZA

Pambano la kombe la shirikisho barani Afrika kati ya Yanga na timu ya Mc Alger ya nchini Algeria kuna uwezekano mkubwa wa kuchezwa mkoani Mwanza kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa baadhi ya viongozi wa klabu ya Yanga.

Baadhi ya viongozi ambao hawakupenda kutajwa majina yao walisema kwamba hadi kufiki sasa mkaguzi wa uwanja kutoka shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF kutoka nchini Malawi yupo jijini Mwanza na ameshakagua na asilimia 99 ameridhika na mambo yote.

Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa kutoka TFF,inasema kwamba uwanja huo kwa siku hiyo utakuwa na ratiba nyingine za kijamii,lakini uongozi wa Yanga umedai kuwa hilo swala halina hofu kwao,kwani Yanga ni muhimu kuliko shughuli hiyo itakayofanyika siku husika.

No comments