CAF YAKATAA YANGA NA MC ALGERS KUCHEZA MWANZA

Uongozi wa klabu ya Yanga umethibitisha mchezo wao wa kimataifa wa kombe la shirikisho barani Afrika dhidi ya MC Algers sasa utachezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Awali kulikuwepo na taarifa kuwa mchezo huo ungechezwa jijini Mwanza lakini kufuatia klabu ya Yanga kuchelewesha kuwasilisha mabadiliko ya uwanja CAF,shirikisho hilo limeshindwa kutoa idhini kutumika kwa uwanja huo kwani uwanja unaotambulika ambao uliwasilishwa na klabu hiyo ni uwanja wa Taifa.

Yanga itashuka dimbani kumenyana na MC Algers siku ya tarehe 8 ya mwezi wa nne mwaka huu katika mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika ambapo mshindi wa jumla atafuzu kucheza hatua ya makundi.

No comments