MOHAMMED DEWJI AENDELEA KUWA BILIONEA KIJANA AFRIKA,DANGOTE AONGOZA KWA UTAJIRI

Mfanyabiashara kutoka Nigeria Aliko Dangote bado ndiye mtu tajiri zaidi barani Afrika kwa mujibu wa orodha ya mabilionea mwaka 2017 iliyoandaliwa na jarida la Forbes.


Kwa mujibu wa taarifa iliyoelezwa na BBC,Utajiri wa Dangote unakadiriwa kuwa jumla ya $12.2 bilioni.


Kuna mabilionea (wa Dola) 25 mwaka huu barani Afrika, mmoja juu ya 24 waliokuwepo mwaka jana.


Wafanyabiasha kutoka Nigeria Femi Otedola na Abdulsamad Rabiu hawakufanikiwa kuingia kwenye orodha hiyo mwaka huu.
Mtanzania Mohammed Dewji bado ndiye bilionea wa umri mdogo zaidi Afrika, utajiri wake ukikadiriwa kuwa $1.09 bilioni.


Isabel dos Santos kutoka Angola na mfanyabiashara wa mafuta Folorunsho Alakija kutoka Nigeria ndiye mabilionea wanawake pekee katika orodha hiyo mwaka huu.


Bw Dangote Dangote, ndiye mwanzilishi na mwenyekiti wa kampuni ya Dangote Cement inayoongoza kwa kuzalisha saruji Afrika. Anamiliki asilimia 90 ya hisa za kampuni hiyo.


Dangote Cement huzalisha tani 44 milioni za saruji kila mwaka na imepanga kuongeza uzalishaji kwa asilimia 33 kufikia 2020.


Dangote pia anamiliki hisa katika kampuni za chumvi, sukari na unga.
Mohammed Dewji ni afisa mkuu mtendaji wa kampuni ya METL iliyoanzishwa na babake miaka ya 1970. 

Kampuni hiyo huhusika katika biashara ya nguo, unga, vinywaji na mafuta. Kampuni hiyo huendesha shughuli zake katika zaidi ya mataifa sita barani Afrika.
Mabilionea 25 wa Afrika mwaka 2017:


1. Aliko Dangote, NigeriaUtajiri: $12.2 bilioni
2. Nicky Oppenheimer, Afrika KusiniUtajiri: $7 bilioni
3. Mike Adenuga, NigeriaUtajiri: $6.1 bilioni
4. Johann Rupert, Afrika KusiniUtajiri: $6.3 bilioni
5. Nassef Sawiris, MisriUtajiri: $6.2 bilioni
6. Christoffel Wiese, Afrika KusiniUtajiri: $5.9 bilioni
7. Nathan Kirsch, SwazilandUtajiri: $3.9 bilioni
8. Naguib Sawiris, MisriUtajiri: $3.8 bilioni
9. Isabel dos Santos, Angola
Utajiri: $3.1 bilioni
10. Issad Rebrab, Algeria
Utajiri: $3 bilioni
11. Mohamed Mansour, MisriUtajiri: $2.7 bilioni
12. Koos Bekker, Afrika KusiniUtajiri: $2.1 bilioni
13. Allan Gray, Afrika KusiniUtajiri: $1.99 bilioni
14. Othman Benjelloun, MoroccoUtajiri: $1.9 bilioni
15. Mohamed Al Fayed, MisriUtajiri: $1.82 bilioni
16. Patrice Motsepe, Afrika KusiniUtajiri: $1.81 bilioni
17. Yasseen Mansour, MisriUtajiri: $1.76 bilioni
18. Folorunsho Alakija, Nigeria
Utajiri: $1.61 bilioni
19. Aziz Akhannouch, MoroccoUtajiri: $1.58 bilioni
20. Mohammed Dewji, Tanzania
Utajiri: $1.4 bilioni
21. Stephen Saad, Afrika KusiniUtajiri: $1.21 bilioni
22. Youssef Mansour, MisriUtajiri: $1.15 bilioni
23. Onsi Sawiris, MisriUtajiri: $1.14 bilioni
24. Anas Sefrioui, MisriUtajiri: $1.06 bilioni
25. Jannie Mouton, Afrika KusiniUtajiri: $1 bilioni

No comments