MASHINDANO YA REDE YASHIKA KASI , TANGA.


NA  BONIFACE  GIDEON, TANGA
Mashindano  ya  mchezo  wa Rede  mkoani  tanga  yanatarajiwa  kuendelea  wiki  hii  baada  ya  kusimama kwamuda.


Hayo  yameelezwa  na Mustahiki  meya  wa  jiji  la  tanga mh.  Mustafa  Seleboss wakati akizungumza  na MWANDIKE.BLOGSPOT, alisema  kuwa  ameamua  kudhamini  mashindano  hayo  kwaajili  ya  kuhamasisha  jamii  kufanya mazoezi na  pia  kuujulisha  umma  kuwa  michezo  ni ajira.


Aliongeza  kuwa  mashindano  hayo  ya  mchezo  wa  rede  amepanga  yafanyike  kila  siku  ya jumapili  na kila timu  inakuwa na  wachezaji watano  na  kwamba  timu  itakayoibuka  na  ushindi  itajipatia  TSH 100,000 .


Aliongeza  kuwa  ameamua  kuanza  kudhamini  kwenye kata  yake  ya nguvumali  ili  kupata  hamasa  kubwa zaidi  na endapo  mashindano  hayo yatapa hamasa kubwa  basi  ataongeza  maeneo  mengine  zaidi'' ndugu mwandishi  mashindano  ya redeyanapendwa sana  na akinamama  na mimi  nimeamua  kudhamini  mchezo huu  ili  kuwahamasisha  akinamama kufanya  mazoezi  ili kuimarisha  afya  zao lakini  pia kujiongezea  kipato kwani  natoa  zawad kubwa ukilinganisha na  aina  ya  mchezo  wenyewe.


Aidha  aliwataka  wadau  wa  michezo  hapa  jijini  tanga  kujitokeza  kwawingi kushuhudia  mashindano hayo kila  jumapili maeneo ya  nguvumali.

No comments