NCHEMBA AKASIRISHWA NA WANAMICHEZO WASIO TAMBUA UMUHIMU WA BENDERA YA NCHI



Waziri wa mambo ya ndani Mwigulu Nchemba amewataka viongozi wa vilabu vya ligi kuu pamoja na shirikisho la mpira wa miguu hapa nchini TFF,kuweza kupanga utaratibu wa kuwaelimisha mashabiki wao kuheshimu bendera ya Taifa pindi klabu ama timu za Taifa zinapocheza katika michuano mbalimbali ya kimataifa

Nchemba ameyasema hayo kufuatia kutoridhishwa na baadhi ya mashabiki wa hapa nchi kuweza kuzomea wakati bendera ya Tanzania inapandishwa katika mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika kati ya Yanga na TP Mazembe mechi iliyopigwa kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam

Amesema kwamba ni vyema mashabiki wakatambua umuhimu wa bendera ya nchi kwani wazee wetu walipigania kwa nguvu kubwa kupata uhuru wa Tanzania,hivyo inashangaza kuona mtanzania unazomea wakati bendera yako ya nchi inapandishwa huku ukishangilia bendera ya nchi nyingine inapopandishwa

Hata hivyo amewataka watanzania kuiga mfano wa mchezaji Mbwana Samata ambae alionyesha uzalendo wa nchi yake wakati timu yake za zamani ya TP Mazembe ilipotwaa taji la ubingwa wa ligi ya mabingwa barani Afrika ambapo baada ya mechi kumalizika alionekana kubeba bendera ya Tanzania mbele ya uma wa watu kutoka nchi tofauti.

No comments