YANGA KUJIPIMA NGUVU NA TIMU YA KMC

Kikosi cha timu ya Yanga siku ya jumapili kinataraji kushuka dimbani kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya KMC inayoshiriki ligi daraja la kwanza.

Afisa Habari msaidizi wa Yanga,Godlsiten Anderson Chicharito amesema kwamba mchezo huo utachezwa kwenye uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi.

Chicharito alisema kwamba kocha mkuu wa timu hiyo anataraji kuutumia mchezo huo kuwaweka sawa wachezaji wake hasa baada ya kusimama kwa ligi kupisha mchezo wa kirafiki kwa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars.

No comments