RAGE ASEMA ENDAPO YANGA WATAENDELEA NA MSIMAMO WAO WA KUWACHEZESHA WACHEZAJI WAPYA BASI WAJIANDAE NA SWALA LA KUPOKWA POINTI

                                                           ISMAIL ADENI RAGE
Aliyewai kuwa mwenyekiti wa klabu ya Simba,Ismail Adeni Rage amewatahadharisha viongozi wa timu ya Yanga kutowatumia wachezaji wapya ambao wamesajiliwa msimu huu akiwemo mchezaji Hassani Ramadhani Kessy kwenye michuano  ya kombe la shirikisho barani Afrika hadi hapo TFF itakapotoa leseni kwa wachezaji wapya ambao wamesajiliwa msimu huu

Rage amesema kwamba endapo kama Yanga watajalibu kuwatumia wachezaji hao basi huenda wakumbana na swala la kupokwa pointi kama ambavyo yeye alifanikiwa kuiondoa TP MAZEMBE kwa kumchezesha mchezaji ambae alikuwa hana sifa za kuichezea timu hiyo

Amesema kwamba tatizo lilipo halipo kwa upande wa timu ya Simba juu ya mchezaji Hassani Kessy ispokua ni mfumo  wa ligi yetu ya Tanzania kwa sababu usajili bado unaendelea na wachezaji wapya bado hawajasajiliwa

Aidha amesema kwamba katika mashindano hayo mchezaji anaeruhusiwa kucheza ni yule mchezaji mwenye leseni ya nchi yake lkn hadi hivi sasa TFF bado haijakaa na kutoa leseni kwa wachezaji wapya ksb usajili bado unaendelea

Hata hivyo amesema kwamba hadi siku ya jana amesoma sheria za CAF na amedai kua hakuna marekebisho yeyote juu ya sheria hiyo hivyo amewaasa viongozi wa Yanga wakajalibu kuwatumia wanasheria wao kuzisoma vizuri kanuni hizo ambazo zinapatikana hata katika tovuti ya CAF,WWW.CAF ON LINE

No comments