SIMBU AIPEPERUSHA VYEMA BENDERA YA TANZANIA

Mwanariadha kutoka Tanzania,Alphonce Simbu amefanikiwa kushika nafasi ya tatu na kubeba medali ya shaba katika mashindano ya dunia ya IAAF yanayofanyika jijini London, Uiengereza.

Simbu ameshika nafasi hiyo baada ya kukimbia kwa saa 2 na dakika 9 na sekunde 51.

Nafasi ya kwanza imeshikwa na Geoffrey Kipkorir KIRUI kutoka nchini Kenya aliyekimbia kwa saa 2 na dakika 8 na sekunde 29 huku nafasi ya tatu ikishikwa na Tamirat Tola kutoka nchini Ethiopia aliyekimbia kwa saa 2 dakika 9 na sekunde 49.

No comments