JKT RUVU WAUKUBALI KWA SHINGO UPANDE MKATABA WA AZAM MEDIA


Meneja wa timu ya JKT RUVU ya Kibaha mkoani Pwani,Duncan Beno amesema kwamba udhamini  wa Azam Media wa bilioni 23 juu ya kupewa haki ya kuonyesha matangazo ya mpira wa miguu katika michezo ya ligi kuu ya Tanzania bara bado ni mdogo kutokana na gharama za uendashaji ligi kua mkubwa

Akiongea na Saidaalymwandike.blogsport Beno amesema kwamba klabu zinatumia kiasi kikubwa cha fedha kuweza kufanikisha kuendesha timu hivyo bado udhamini huo haukidhi matakwa ya vilabu katika uendeshaji wa timu

Hata hivyo amedai kua maamuzi ya makubaliano ya mkataba huo kwa kiasi kikubwa wao hawakuhusika kwani liliopangwa na TFF ndilo lililopitishwa ingawa baadhi ya klabu hazikulizishwa na mkataba huo wa miaka mitano wenye thamani ya bilioni 23

No comments