AZAM WAPANGA KUSAJILI WACHEZAJI 4 KUTOKA NJE YA NCHI


Wakati dirisha la usajili wa wachezaji likitarajiwa kufungwa,Mtendaji mkuu wa timu ya Azam,Saad Kawemba amesema kwamba msimu huu uongozi wa klabu hiyo umepanga kufanya usajili wa wachezaji wanne kutoka nje ya nchi na hawana mpango wowote wa kusajili mchezaji wa hapa nyumbani kwa kua wachezaji waliopo ndani ya klabu hiyo ni bora kuliko wachezaji wote wa hapa nyumbani

Akiongea na Mwandike.blogsport Kawemba amesema kwamba kwa sasa wamefanikiwa kupandisha wachezaji wanne wa timu ya vijana ya Azam ambao hawa wataungana na wachezaji wanne wapya watakaosajiliwa kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu ya Tanzania bara

Kawemba amesema kwamba msimu ujao wanatarajiwa kuwa na jumla ya wachezaji 44 ambapo wachezaji 22 watakua kikosi cha kwanza na 22 ni wachezaji wa timu ya vijana

No comments