AZAM TV YAINGIA MKATABA WA MIAKA 5 WENYE THAMANI YA BILIONI 23 KWA AJILI YA KURUSHA MECHI ZA LIGI KUU YA TZ BARA



Kampuni ya Azam Media imeingia mkataba wa kurusha matangazo ya ligi kuu ya Tanzania bara wenye thamani ya bilioni 23 kwa kipindi cha miaka mitano mara baada ya kufanikiwa kuyapiku makampuni mengine ambayo nayo yalionyesha nia ya kutaka kuingia mkataba wa kuonyesha mechi za ligi kuu ya Tanzania bara

Akiongea mbele ya waandishi wa Habari leo hii katika ofsi za TFF,Mkurugenzi wa kampuni ya Azam Media Tiddo Muhando amesema kwamba kwa upande wao wamefarijika kuwa washindi wa umiliki wa matangazo hayo kwani nia yao ni kuona wanaleta chachu ya maendelea katika mpira wa miguu hapa nchini

Amesema kwamba mara baada ya kufanikiwa jambo hilo sasa kilichopo ni kuhakikisha kua msimu ujao matangazo yao yanakua bora tofauti na misimu mitatu ya nyuma

 Nae mtendaji mkuu wa bodi ya ligi,Boniphace Wambura amesema kwamba mkataba huo ambao wenye thamani ya bilioni 23 kwa miaka mitano ni tofauti na mkataba wa awali ambao huu wa sasa umekua na maboresho makubwa ambayo yatazifanya vilabu shiriki kwenye michuano hiyo kuleta ushindani wa kutosha

Amesema kwamba vilabu vingi vimekua havileti ushindani wa kutosha kutokana na ukata wa fedha hivyo kwa mkataba huu anaamini kwa kiasi kikubwa fedha hizo zitakua na manufaa kwa upande wao

Aidha amedai kua mgawanyo wa fedha hizo utagawanywa katika awamu nne ambapo awamu ya kwanza hadi ya tatu kila klabu itapata milioni 42 huku awamu ya nne mara baada ya ligi kumalizika mgawanyo utakua mkubwa kwa timu ambazo zimeshika nafasi ya juu kwenye msimamo wa ligi

No comments