KOCHA MSAIDIZI AIPONZA SIMBA

Klabu ya wekundu msimbazi Simba imepewa onyo kali na imetakiwa kujieleza kwa kina kutokana na klabu hiyo kumtumia kocha wao msaidizi Massoud Djuma kukaa katika benchi pasipo kuwa na vibali vya kufanya kazi hapa nchini.

Mtendaji mkuu wa bodi ya ligi,Boniphace Wambura alisema kwamba maelekezo hayo kwa klabu ya Simba yamezingatia kanuni za uendeshaji wa bodi ya ligi na TFF kwa ujumala.

Wambura alisema kwamba,mbali na onyo hilo pia klabu ya Simba imepigwa faini ya shilingi laki tatu kwa kitendo chao cha kushindwa kuwasilisha mapema orodha ya majina ya wachezaji katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania bara dhidi ya Njombe Mji.

No comments