AIRTEL YAKABIDHI VIFAA KWA TIMU ZA VIJANA KWA AJILI YA MASHINDANO YA AIRTEL RISING STAR




Kampuni ya simu za mkononi Airtel,leo hii imekabidhi vifaa vya michezo zikiwemo jezi kwa timu ambazo zinashiriki michuano ya vijana ya Airtel Rising Star inayotaraji kuanza kutimua vumbi siku ya jumamosi kwa ngazi ya mkoa

Akiongea na MWANDIKE.BLOGSPORT,meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mbano amesema kwamba vifaa hivyo vya michezo ambavyo vitatumika katika mashindano hayo kwa timu zote vina thamani ya shilingi milioni 200


Mbando amesema kwamba mgeni rasmi katika ufunguzi wa mashindano hayo ambayo yatazinduliwa kwenye uwanja wa Karume katika makao makuu ya TFF anatarajiwa kua mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paulo Makonda sambamba na viongozi wengine wa mpira wa miguu hapa nchini.

Amesema kwamba dhamira yao ni kuona kampuni ya Airtel inasaidia kukuza vipaji vya vijana kupitia sekta ya michezo kama ambavyo wamekua wakifanya kipindi chote ambacho wamekua wakidhamini mashindano ambayo yamefanikiwa kuibua vipaji bora vya vijana ambao kwa sasa wamekua msada mkubwa kwa timu za taifa hasa katika kikosi cha Serengeti boys.
Kwa upande wake katibu mkuu wa TFF,Mwesigwa Selestine ameishukuru kampuni hiyo kwa kuendelea kutoa udhamini kwa timu za vijana ambapo kwa mujibu wa taarifa yake amesema kwamba Airtel imekua msada mkubwa kwa kuibua vipaji vya vijana katika sekta ya michezo hivyo amewataka wadau wengine nao waige mfano huo ili kuendelea kuleta chachu ya  maendeleo ya soka hapa nchini


Mwesigwa amesema kwamba jambo ambalo linafanywa na Airtel ni jambo zuri linalotakiwa kuigwa na makampuni mengine kwa ajili ya kuwekeza katika mashindano mbalimbali,pia amewataka mashabiki wa mpira kuendelea kutumia mtandao wa kampuni hiyo ikiwa ni pamoja na kununua vocha kwani kufanya hivyo ni sawa na kuipa sapoti kampuni hiyo iendelee kudhamini mashindano hayo ya Airtel Rising Star.

No comments