DONALD NGOMA AIKANA SIMBA SC

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Yanga,Donald Ngoma amerejea nchini akitokea nchini Afrika ya Kusini ambako alikwenda kwa ajili ya matibabu.

Uongozi wa Yanga ulichukua jukumu la kumpeleka mchezaji huyo kutibiwa nchini Afrika ya Kusini baada ya kukumbwa na majeraha ya mara kwa mara ambayo yalishindwa kumpa nafasi ya kucheza vizuri tangu mwezi wa kwanza mwaka huu.

Taarifa zilizopo ni kwamba baada ya kurejea hapa nchini itamchukua miezi mitatu mchezaji huyo ili kupona kabisa na kuanza kuitumikia timu hiyo ya Yanga.

Aidha katika hatua nyingine Ngoma alisema kwamba  kwa sasa yeye yupo tayari kuitumikia klabu hiyo msimu mwingine mmoja baada ya mkataba wake wa awali kuelekea ukiongoni kwa madai ya kutaka kulipa fadhila kwa klabu hiyo.

Hata hivyo ameshangazwa na taarifa zinazoeleza kuwa yeye amesaini klabu ya Simba akidai kuwa hakuna kitu kama hicho na amedai kuwa hawezi kucheza timu nyingine hapa nchini zaidi ya Yanga hivyo anaamini ikishindindikana ni bora arejee katika timu yake ya zamani ya FC Platnum.

No comments