VIONGOZI WA MATAWAI WAMKATAA AKILIMALI WATAKA ASIMAMISHWE UWANACHAMA




Baadhi ya viongozi wa matawi wa klabu ya Yanga mkoa wa Dar es salaam pamoja na wanachama kwa pamoja wametoa lawama zao kwa katibu mkuu wa baraza la wazee wa klabu hiyo,Ibrahim Akilimali kwa kusema kwamba katibu huyo ndiye anayeleta mvuragano kwenye timu hiyo kufuatia kutoa kauli za uchochezi kwenye vyombo vya habari hasa zikimlenga mwenyekiti wao Yusuph Manji

Akiongea mbele ya waandishi wa Habari kaimu mwenyekiti wa kanda zote za Dar es salaam Robert Ilyungukasere amesema kwamba kama wao viongozi wa matawi wameamua kufanya hivyo baada ya kuwepo kwa taarifa za kutaka kujiuzulu kwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuph Manji na kusitisha mpango wake wa kutaka kuikodisha timu kwa miaka 10

Amesema kwamba kwa sasa kwa pamoja wameutaka uongozi wa klabu hiyo kupitia kwa katibu mkuu wa klabu kumuondoa Akilimali katika wadhifa wake wa kua katibu mkuu wa baraza la wazee kwa kua yeye ndio kikwazo kikubwa kwa sasa kuhusiana na swala hili ambalo limemuhudhunisha Zaidi Manji

Nae mwenyekiti wa tawi la mwembe Yanga, Jamali Tail ameutaka uongozi wa klabu hiyo kumfuta uwanachama wa klabu hiyo Ibrahim Akilimali kwani amekua hana msada ndani ya klabu hiyo isipokua amekua akileta mvurugano kwa vipindi tofauti

"Akilimali ashawai kutoa kauli yake ambayo ikapelekea tukafungwa goli tano na simba na leo hii ameendea kuleta mgogoro wakati kesho tuna mechi ya ngao ya jamii dhidi ya Azam" alisema Jamal Tail.

Amesema kwamba Akilimali amekua akizungumza kauli ambazo mara nyingi zimekua na athari kubwa kwa timu ikiwemo hivyo jambo zuri la kufanya kwa sasa ni kutomtambua katibu huyo kama ni kiongozi wa Yanga kupitia baraza la wazee

Aidha amemtaka mwenyekiti wa klabu Yusuphu Manji kupuuzia jambo hili kwani mara nyingi hua mwadamu hakubaliki na watu wote ingawa anafanya jambo jema.

No comments