CAF YASIMAMISHA KOZI ZOTE ZA SOKA

Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF limesitisha kozi zote zinazosimamiwa na shirikisho hilo ambazo zilikuwa zinaendelea ili kufanya mapitio kwa kozi zote zilizopita.

Mkurugenzi wa ufundi wa TFF,Salum Madad alisema kwamba kutokana na agizo hilo kutoka CAF,nalo shirikisho la mpira wa miguu hapa nchini TFF limeamua kusimamisha kozi zote ikiwemo ya ukocha  ya leseni C iliyokuwa inaendelea kufanyika mkoani Morogoro hadi hapo watakapopata maagizo mengine.

Madad amewataka washiriki wa kozi hiyo kukubaliana na hali hiyo kwani ni maagizo ambayo yametolewa na chombo kikuu cha uendeshaji wa soka barani Afrika.

No comments