YANGA LIFE WAWAJAZA FEDHA WACHEZAJI WALIOFANYA VIZURI

Group la WhatsApp la ‘Yanga for life’, likiwakilishwa na msanii wa filamu nchini, Vicent Kigosi, ‘Ray’, wametoa zawadi ya fedha, viatu na ‘shin gard’, kwa wachezaji watatu, waliofanya vizuri katika michezo ya Ligi.

Straika Ibrahim Ajib, amepewa kiasi cha Tsh Milioni moja, baada ya kuibuka nyota wa mchezo kwenye mechi mbili, Kagera na Stand United.

Papy Kabamba Tshishimbi, aliyechagulia nyota wa mchezo wa ‘Derby’, dhidi ya Simba, amekabidhiwa Tsh 500, 000 huku kipa Youthe Rostand, akipata Tsh 200,000, viatu na ‘shin gard’.

“Tunafanya hivi kwa ajili ya kuwapa hamasa wachezaji wetu. Kwa Mwanayanga yeyote atakayependa kujiunga na kundi letu, atutafute kwa namba 0717 554545. Lengo letu ni kuiona timu yetu inafanya vizuri na kutwaa ubingwa mara nne mfululizo,” alisema Ray.

Hii si mara ya kwanza kwa group hilo kutoa motisha kwa wachezaji,kwani awali walishafanya hivyo kwa mchezaji Kelvin Yondani baada ya kuonekana alikua mchezaji bora katika baadhi ya mechi za ligi kuu ya Tanzania bara.

No comments