WAZEE SIMBA WAMKATAA MOHAMED DEWJ

Wazee wa klabu ya Simba kupitia kikao cha hii leo kwa pamoja wameazimia kwenda kumuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli ili kumueleza kilio chao baada ya kugundua kuwa kuna shinikizo kutoka kwa baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali wakihitaji klabu hiyo auziwe Mohamed Dewji.

Akiongea mbele ya waandishi wa Habari mratibu wa wazee wanachama wa Simba Felix Makuwa alisema kwamba wazee hao kwa upande wao hawana imani na Mohamed Dewji kwani ndie analeta mvurugano usiokuwa na tija ili afanikiwa kuinunua timu.

Nae mwanachama wa klabu hiyo Chuma Suleiman maarufu kwa jina la Bi hindu ameendelea kusisitiza swala hilo akitaka Rais Magufuli awasaidie kwenye jambo hilo kwani wanahisi kuna chembechembe za rushwa zenye lengo la kuidhohofisha Simba.

No comments