HANS POPE AJIUZULU SIMBA SC

Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu ya Simba,Hans Pope amejiuzulu rasmi uongozi ndani ya klabu hiyo  kwa kile kinachoelezwa kuwa hakufurahishwa na hatua zilizochukuliwa na baadhi ya viongozi wa klabu hiyo kuingia mkataba wa miaka mitano na kampuni ya SportPesa.

Taarifa zinaeleza kuwa Hans Pope hakuridhishwa na mchakato wa uingiaji wa mkataba huo ikiwemo kushindwa kumshirikisha hata Mohamed Dewji ambae alikuwa akilipa mishahara kwa wachezaji wa Simba.

Kampuni ya SportPesa imeingia mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya bilioni 4.9 kuidhamini Simba ambapo makubaliano hayo yamefanywa na Raisi wa Simba Evans Aveva.

No comments