TFF WAUKATAA MFUMO WA UKODISHWAJI NDANI YA KLABU YA YANGA



Shirikisho la mpira wa miguu hapa nchini TFF limesema kwamba kwa sasa bado hawatambui mabadiliko yaliyofanyika ndani ya klabu ya Yanga ya mfumo wa kukodisha timu kwa muda wa miaka 10 kwa kampuni iliyopewa jina la Yanga yetu.

Akiongea mbele ya waandishi wa Habari leo hii katibu mkuu wa TFF,Mwesigwa Selestine amesema kwamba kwa mujibu wa taratibu za klabu ya Yanga TFF inaendelea kutambua mfumo wa awali wa uendeshaji na sio huu unaozungumzwa na vyombo mbalimbali vya habari kwani bado shirikisho hilo halijapelekewa barua inayoelezea mabadiliko hayo.

Amesema kwamba Yanga ni klabu ya wanachama hivyo kile ambacho kinapaswa kufanyiwa marekebisho ni vyema kifuate misingi na katiba ya klabu hiyo ili chini ya mwenyekiti Yusuph Manji.

Katika hatua nyingine Mwesigwa amesema kwamba shirikisho hilo limeiandikia barua klabu ya Yanga ili kupata ufahamu wa jinsi mchakato wao wa mabadiliko ulivyofanyika.

Mwesigwa amesema kwamba TFF imeomba nakala kwa katibu mkuu wa klabu hiyo ili kufahamu vizuri mkataba wa ukodishwaji na waweze kuupitia ili kama una mapungufu yaweze kufanyiwa kazi kwani Yanga ni klabu ya wanachama hivyo mpangilio wa uendeshaji wa klabu ukiwa mbaya basi huenda kukawa na athari kubwa kwa wanachama wa klabu hiyo.

No comments