MWAISABULAH AMKINGIA KIFUA KOCHA HANS
Mchambuzi wa mpira wa miguu hapa nchini Kenny Mwaisabulah amesema kwamba uongozi wa Yanga utafanya kosa kubwa endapo utachukua jukumu la kufanya mabadiliko kwenye benchi la ufundi kwani kwa sasa makocha hao wanapaswa kusalia ndani ya klabu hiyo iliyoingia kwenye mchakato wa mabadiliko ya kiutawala.
Mwaisabulah
 amesema kwamba kwa sasa benchi la ufundi la Yanga ni vyema likaendelea 
kusalia ndani ya klabu hiyo kwani kwa muda mrefu wamekaa pamoja na 
wachezaji na hata kiwango chao cha ufundishaji bado kinaridhisha.
Amesema
 kwamba huenda uongozi wa Yanga ukafanya jambo hilo baada ya kutopata 
matokeo mazuri katika pambano lao la watani wa jadi dhidi ya Simba 
lakini kwa mtazamo wake makocha hao bado wana mchango mkubwa ndani ya 
timu na kwake haoni makosa yanayofanywa na makocha hao hasa kocha mkuu 
anayenyoshewa kidole na baadhi ya mashabiki wa klabu hiyo.

Post a Comment