WANACHAMA WA YANGA WAMPA TIMU MANJI KWA MIAKA KUMI



Wanachama wa  klabu ya Yanga kwa pamoja wamekubali kumkodisha klabu hiyo Mwenyekiti wao, Yusuf Manji kwa miaka 10 kuanzia leo ambapo katika kipindi hicho yeye atakua na haki ya kumiliki timu pamoja na nembo ya klabu

Uamuzi huo umefikiwa katika Mkutano Mkuu wa dharula uliofanyika leo katika ukumbi wa Diamond jubilee, Dar es Salaam ambapo Manji ameomba apewe klabu kwa miaka 10 na katika kipindi hicho atakuwa anachukua asilimia 75 ya mapato ya timu, huku asilimia 25 ikibaki kwa wanachama.
Aidha katika hatua nyingine amesema kwamba swala la kujenga uwanja wa klabu jambo hilo kwa sasa ni gumu lakini baada ya kupata idhini ya kumiliki nembo na timu atahakikisha kua atafanya jitihada kubwa kuzungumza na viongozi wa TFF juu ya maswala ya haki ya matangazo ya televisheni akidai kua hilo ndio tatizo linalopelekea uongozi kushindwa kujenga uwanja kwa kua mapato ni madogo

Amesema kwamba vitega uchumi vya klabu yakiwemo majengo vitaendelea kua mali ya wanachama na hivyo wao watakua na idhini ya kumkodishia endapo wataridhia kufanya hivyo kwa kipindi chote cha miaka 10

Nae  Mjumbe wa Baraza la Wadhamini la klabu, Francis Kifukwe amesema  kwamba baada ya wanachama kuridhia mpango huo, wao wanampa pia ridhaa hiyo Manji ya kuiongoza timu kwa miaka 10

Hata hivyo amedai kua kilichopo sasa ni baraza hilo la wadhamini kufanya jambo hilo haraka kama alivyohita Manji ili mchakato huo uanze kutumika


No comments