WADHAMINI WA LIGI KUU WAKABIDHI VIFAA KWA TIMU SHIRIKI ZA LIGI KUU YA TANZANIA BARA



Timu ambazo zinashiriki ligi kuu ya Tanzania bara,zimekabidhiwa vifaa mbalimbali na mdhamini mkuu wa ligi hiyo,vifaa ambavyo vimekabidhiwa kwa timu shiriki vina thamani ya Zaidi ya shilingi milioni 514

Akiongea katika hafla hiyo ya utoaji vifaa mtendaji mkuu wa bodi ya ligi,Boniphace Wambura ameishukuru kampuni hiyo,na kuzitaka klabu shiriki kuheshimu chapa ya mdhamini wakati wote wa mechi za ligi

Amesema kwamba kwa upande wa Bodi ya ligi maandalizi kwa ujumla yamekamilika ikiwemo waamuzi kupata semina kabla ya kuanza kwa michuano hiyo ambapo ufunguzi rasmi utafanyika siku ya tarehe 17 ambapo kutakua na mechi kati ya mabingwa watetezi wa kombe hilo,timu ya Yanga itakapomenyana na makamu bingwa Azam.


Wambura amesema kwamba anaamini msimu huu ligi itakua bora baada ya kufanya maandalizi mazuri huku akiwasifu waamuzi wa msimu uliopita kwamba walifuata sheria 17 za soka kwa kua hakuna mwamuzi ambae amefungiwa hivyo msimu huu watakua bora Zaidi

Hata hivyo amesema kwamba katika ligi ya msimu huu kuna baadhi ya mechi zitachezwa kwenye uwanja wa Uhuru kwa baadhi ya timu za Dar es salaam na uwanja mkuu wa Taifa utatumika kwa mechi zenye washabiki wengi

No comments