AZAM WAENDELEA KUZITAKA YANGA NA SIMBA ZICHEZE AZAM COMPLEX



Uongozi wa mabingwa wa ngao ya Hisani timu ya soka ya Azam ya jijini Dar es salaam,umesema kwamba umepokea taarifa kutoka shirikisho la mpira wa miguu hapa nchini TFF juu ya mpango wao wa kutaka mechi zao za ligi kuu ya Tanzania bara ambazo watacheza na Yanga pamoja na Simba ziweze kuchezwa kwenye uwanja wao wa Azam Complex.

Msemaji wa timu hiyo Jafari Idd amesema kwamba katika taarifa yao ambayo wameipata kutoka TFF ni kwamba shirikisho hilo limekataa mpango huo kwa sababu zilizoelezwa ni za kiusalama.

Jafary amesema kwamba anashangaa shirikisho hilo kuwakatalia ombi lao ilihali uwanja wao una vigezo vyote ambavyo vimekamilika sambamba na kupitishwa na shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF juu ya uwanja huo utumike kwenye mechi za mashindano.

Amesema kwamba sababu iliyotolewa na TFF haina mashiko kwani jukumu la kiusala linapaswa kufanywa na jeshi la Polisi ambao wao ndio wenye mamlaka juu ya jambo hilo.

Aidha uongozi wa klabu hiyo umesema kwamba utalitolea ufafanuzi swala hilo pindi watakapomaliza mechi zao zijazo za ligi ikiwemo ya Majimaji inayotaraji kupigwa siku ya jumamosi pamoja na mechi zinazofuata watakazocheza mkoani Mbeya.

No comments