SIMBA YAMALIZA UTATA SWALA LA KOCHA OMOG

Uongozi wa timu ya soka ya Simba SC umemaliza uzushi uliokuwa ukiendlea kuwa klabu hiyo imetoa mechi 5 kwa kocha Joseph Omog ili iweze kumtimua kazi.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na MWANDIKE.BLOGSPOT,Mjumbe wa kamati tendaji wa klabu hiyo Said Tulliy alisema maneno hayo ya kumpa michezo mitano kocha huyo wa Cameroon ni uongo na hawajui nani kaanzisha.
‘’Ni uzushi mtupu hatutamtimua kocha wetu Joseph Omog,Habari rasmi lazima itokee kwa klabu yetu tunaomba wadau,wapenzi pamoja na wanachama wasisikilize maneno haya bali wayapuuze’’Tulliy alisema.
Akielezea kuhusu matokeo ya timu yao,Tulliy alisema mpaka sasa timu yao haijafanya vibaya katika ligi kwa kuwa imecheza michezo minne na imeshinda miwili dhidi ya Ruvu shooting na Mwadui. Huku ikiwa imetoka sare ugenini dhidi ya Mbao FC na Azam FC.
Tulliy alisema walimu wao wote wawili Jackson Mayanja na Joseph Omog wanafanya kazi nzuri sana na uongozi wao una imani kuwa watafanya vyema katika msimu huu wa ligi kuu.
Kwa upande wake msemaji wa timu ya soka ya Simba SC Haji Manara alisema timu yao ina imani kubwa sana na kocha Omog kwa mafanikio aliyowapa.
Manara alisema watu wasiopenda klabu yao wamekuwa wakizusha uvumi kuwa timu yao itamfukuza kocha huyo jambo ambalo si jema.

No comments