REAL MADRID YASHIKWA SHATI IKIWA UGENINI


Klabu bingwa barani Ulaya imeendelea usiku wa kuamkia leo hii katika viwanja tofauti  ikiwa bado ni hatua ya makundi.
Mchezo wa kusisimua zaidi ukiwa kati ya Legia Warsaw dhidi ya Real Madrid ambao ulikuwa wa piga nikupige.
Huku ikishuhudiwa Gareth Bale akifunga goli la kusisimua zaidi. Matokeo ya mwisho Legia Warsaw 3-3 Real Madrid.
Monaco ikiwa nyumbani imeibuka na ushindi wa 3-0 dhidi ya CSKA ya Moscow.
Tottenham Hotspur pia ikiwa nyumbani katika dimba la Wembley ilikubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Bayer Leverkusen.
Leicester City ikiwa ugenini ililazimishwa sare tasa dhidi ya FC Copenhagen.
Matokeo ya michezo mingine
Borussia Dortmund 1-0 Sporting
FC Copenhagen 0-0 Leicester city
FC Porto 1-0 Club Brugge
Juventus 1-1 Lyon1
Sevilla 4-0 Dinamo Zagreb.


No comments