STEND UNITED WAWEKA BAYANA SIRI YA MAFANIKIO YAO YA KUANZA VYEMA



Uongozi wa klabu ya Stend United ya mkoani Shinyanga umesema kwamba kufanya kwao vizuri  tangu kuanza kwa msimu ni kuwa na maandalizi mazuri kabla ya ligi pamoja na viongozi wa klabu hiyo kuwajenga kisaikolijia wachezaji wa timu hiyo.

Msemaji wa timu hiyo Deo Kaji Makomba ameiambia MWANDIKE.BLOGSPORT kwamba kulikuwa na maneno mengi kutoka kwa baadhi ya wadau wa soka wakidiriki kusema timu hiyo ingeshuka daraja hasa baada ya kuwepo na mgogoro uliyowahusisha viongozi wa Kampuni na wanachama lakini kwa kutambua umuhimu wa timu hiyo wamejizatiti kuiongoza vyema.
 
Aidha katika hatua nyingine Makomba amesema kwamba swala la uendeshaji timu limekuwa tatizo kutokana na fedha zinazotelewa na wadhamini wa ligi hiyo kutokizi matakwa yao ya uendeshaji lakini kama wao viongozi wanaendelea kupigana kuondokana na adha hiyo ya ukata.

Hata hivyo Makomba amekili kuwa kwa sasa uongozi wa klabu hiyo upo katika mazunguzmo na kampuni ya ACACIA kuona ni jinisi gani wanamaliza tatizo lililopo hasa baada ya kampuni hiyo kutangaza kujiondoa kuidhamini timu hiyo baada ya kuwepo na mgogoro hapo awali.
 
"Sisis bado tunatambuwa kuwa mdhamini wetu bado ni ACACIA hivyo kama kuna upande unataka kuvunja mkataba basi ni vyema ukafuata taratibu ikiwemo kutoa notisi na pia kuwepo na maeleano ya uvunjaji wa mkataba huo lakini naamini hilo swala litakwisha kwani tumeshaanza mchakato wa kulitatua tatizo hilo"alisema Makomba.

No comments