VIINGILIO MCHEZO WA AZAM FC v SIMBA SC

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania linapenda kuwatangazia wananchi kuwa viingilio katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Azam na Simba.
Mchezo huo utafanyika Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam na viingilio vitakuwa shilingi elfu kumi (Sh 10,000) kwa Jukwaa Kuu ambalo lina uwezo wa kubeba mashabiki 1,000 tu walioketi, wakati mzunguko (popular) kiingilio kitakuwa ni shilingi elfu saba tu (Sh 7,000).

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania linapenda kuwatangazia wanafamilia ya mpira wa miguu kukata tiketi kuanzia leo Jumatano Septemba 6, mwaka huu ili kujiepusha na usumbufu wa aina yoyote.

Kadhalika tunapenda kuwatangazia wananchi kwamba kwa ye yote ambaye hana tiketi ni vema wasiende uwanjani kwani ujio wake hautakuwa na tafasiri nyingine zaidi ya kuonekana kuwa ni mleta fujo.

Vyombo vya usalama vitakuwa makini kudhibniti kila aina ya vurugu uwanjani hapo hasa ikizingatiwa kuwa mchezo huo utafanyika wakati jua limezama. Mchezo utakuwa Septemba 9, 2017 saa 1.00 (19h00).

No comments