MAAMUZI YA KAMATI JUU YA MCHEZAJI PIUS BUSWITA

Kamati Ya Sheria, Katiba na hadhi za Wachezaji imeridhia ridhaa za timu za Simba na Yanga kuhusu mchezaji Pius Buswita ambaye alisaini katika timu zote mbili.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Elias Mwanjala alisema kwamba vilabu hivyo vilikaa na kwa pamoja vimekubaliana mchezaji ailipe klabu ya Simba fedha ambazo alizichukua.

Mwanjala alisema kwamba kamati hiyo imebaini kuwa mchezaji anatakuwa kuirejeshea Simba shilingi milioni 10 pamoja na ongezeko la milioni moja kama gharama za nauli ndipo aruhusiwe kucheza ligi.

Alisema kwamba klabu ya Simba ilihitaji kulipwa milioni 15 wakidai ndicho kiasi walichompa lakini kamati imeangalia mkataba aliosaini mchezaji ambao unaonyesha alisaini kwa kiasi cha shilingi milioni 10.

Aliongeza kuwa mbali na kurejesha fedha hizo lakini kamati itampa onyo kali mchezji Pius Buswita kwa kitendo ambacho amekifanya cha kusaini katika vilabu viwili.

Hata hivyo alidai kua endapo vilabu hivyo visengekubaliana vyenyewe basi kamati ingekuchukua maamuzi makali kwa wahusika kwani ndani ya usajili huo klabu ya Simba na Mchezaji walishindwa kufuata taratibu za usajili.

No comments