WEST HAM WAMTUPIA VIRAGO MKUFUNZI WA TIMU HIYO

Mkufunzi wa klabu ya West ham Tony Pulis amefutwa kazi na klabu hiyo huku klabu hiyo ikiwa pointi moja tu juu ya eneo la kushushwa daraja mbali na kutopata ushindi hata mmoja katika mechi zake 10 ilizocheza.
West Brom walicharazwa mabao 4 kwa sufuri na mabingwa watetezi wa ligi Chelsea.
Albion waliwezahinda mechi zake tatu za kwanza msimu huu lakini wameweza kutoka sare mechi nne na kupoteza saba tangu ilipoishinda Accrington katika kombe la Carabao 22 mwezi Agosti.
Aliyekuwa mkufunzi wa zamani wa klabu hiyo Gary Megson ambaye alikuwa naibu wa Pulis anachukua mahala pake hadi timu hiyo itakapotoa tangazo jingine.
Mwenyekiti wa klabu hiyo John Williams aliongezea:Uamuzi kama huu hauchukuliwa kwa urahisi lakini kwa sababu ya maslahi ya klabu.
Tuko katika biashara ya kupatamatokeo mazuri lkini kutokana na matokeo mabaya ambayo yamekuwa yakishuhdiwa kufikia mwishoni mwa msimu uliopita na kufikia sasa matokeo yamekuwa mabaya.
West Brom inakutana na Tottenham ika ligi ya Uingereza katika uwanja wa Wembley siku ya Jumamosi.

No comments