TETESI ZA SOKA ULAYA LEO IJUMAA

Real Madrid inamuwania mchezaji wa kiungo cha kati wa Manchester United Paul Pogba msimu huu wa joto, lakini watahitaji kutoa zaidi ya £ milioni 120 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 ambaye ndiye mchezaji aliyevunja rekodi ya usajili alipohamia Old Trafford. (Sun)
Lakini Pogba ana uwajibikaji kuondosha tofuati zozote za kimaono na meneja wa United Jose Mourinho. (Telegraph)
Jitihada za Pogba akiwa ndani ya Manchester United zimepungua baada ya kuwasili kwa mchezaji wa kiungo cha mbele wa Chile Alexis Sanchez, mwenye mri wa miaka 29, kutoka Arsenal, kwa mujibu wa aliyekuwa kapteni wa timu hiyo ya mashetani wekundu Paul Ince. (Mirror)
Mke na mwakilishi wa kapteni wa Inter Milan Icardi, anafanya mazungumzo kujaribu kufikia makubaliano na Manchester United, licha ya mchezaji huyo kuhusishwa na uhamisho wa msimu wa joto kwenda Real Madrid. (Corriere dello Sport via ESPN)
Liverpool inajaribu kufikia makubaliano kumsajili kipa wa Roma Alisson, mwenye umri wa miaka 26, kabla ya kufunguliwa dirisha la uhamisho katika msimu wa joto, lakini raia huyowa Brazil ana thamani ya £milioni 62 na wanakabiliwana ushindani mkubwa wa kutaka kumsajili. (Sky Sports)
Kwa upande mwingine huenda Liverpool ikawacha kumuwania Alisson na kusalia na kipa wa Ujerumani Loris Karius. (Telegraph)
Kipa wa England Joe Hart, mwenye umri wa miaka 30, yuko tayari kujiuzulu Manchester City na ahamie ng'ambo msimu huu wa joto baada ya kutemwa akiwa katika mkopo huko West Ham msimu huu. (Sun)
Malcom, mchezaji wa kiungo cha mbele wa Brazil anayelengwa na Arsenal na Tottenham, amethibitisha ana makubaliano na klabu aliyopo sasa ya Bordeaux yanayomruhusu kuondoka msimu huu wa joto. (UOL via Sky Sports)
Aliyekuwa kapteni wa England John Terry anataka kurudi Chelsea katika jukumu la kuwa kocha anapopanga njia yakurudi katika kazi hiyo kuu huko Stamford Bridge. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 anayecheza kiungo mlinzi anamaliza mkataba wake na Aston Villa mwezi July wakati mkataba wake wa mwaka unapomalizika. (Mirror)
Huenda Tottenham ikafikiria ombi kwa mlinzi wa kimataifa raia wa Ubelgiji Toby Alderweireld, mwenye umri wa miaka 28, msimu huu wa joto lakini wana imani kuwa wataendelea kuwahifadhi wachezaji wote wanaowataka wasalie. (London Evening Standard)

Mazungumzo ya hivi karibuni ya Spurs na mlinzi huyo kutafuta mkataba yaliishia bila maafikiano. (ESPN)

No comments