MASOGANGE AHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA MIWILI

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo hii imemhukumu kwenda jela miaka miwli au kulipa faini ya Shilingi milioni 1.5, Video Queen Agnes Gerald maarufu kwa jina la Masogange kwa kosa la kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin.

Video Queen huyo aliyeanza kutamba baada ya kuonekana katika video ya msanii wa Bongo Flever,Belle 9 katika wimbo uliojulikana kwa jina la Masogange sakata lake liliibuliwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam alipowataja watu maarufu kufika Polisi kwa kujihusisha matumizi ya dawa za kulevya mwezi Februari mwaka jana.

No comments